Proverbs 19:5-10


5 aShahidi wa uongo hataacha kuadhibiwa,
naye amwagaye uongo hataachwa huru.

6 bWengi hujipendekeza kwa mtawala
na kila mmoja ni rafiki wa mtu atoaye zawadi.

7 cMtu maskini huepukwa na ndugu zake wote:
Je, marafiki zake watamkwepa kiasi gani!
Ingawa huwafuata kwa kuwasihi,
hawapatikani popote.

8 dYeye apataye hekima huipenda nafsi yake mwenyewe,
yeye ahifadhiye ufahamu hustawi.

9 eShahidi wa uongo hataacha kuadhibiwa,
naye amwagaye uongo ataangamia.

10 fHaistahili mpumbavu kuishi katika anasa,
itakuwa vibaya kiasi gani
kwa mtumwa kuwatawala wakuu.
Copyright information for SwhNEN